Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kiruddu, Dkt. Charles Kabugo, ametoa wito kwa serikali ya Uganda kujenga hospitali nyingine maalum kwa ajili ya matibabu ya majeruhi wa moto karibu na maeneo ya uzalishaji wa mafuta.
Amesema kuwa ongezeko la shughuli za mafuta linaongeza hatari ya milipuko na ajali za moto, hasa katika wilaya ya Hoima.
Hospitali ya Kiruddu iliyopo Kampala iko umbali mrefu na haiwezi kukidhi mahitaji endapo kutatokea ajali kubwa.
Dkt. Kabugo alisema nchi bado haijajiandaa vya kutosha kushughulikia maafa makubwa ya moto, na pendekezo la kujenga kituo kikubwa zaidi linaandaliwa kuwasilishwa serikalini.
CHANZO: TRT Afrika














