Mechi za mwisho za hatua ya makundi katika Kombe la Mataifa ya Afrika 2025 nchini Morocco zinaanza Jumatatu, huku timu nyingi zikisubiri hatma yao ya kufuzu hatua ya 16 bora.
Hadi sasa, ni timu tatu pekee — Misri, Nigeria na Algeria — zilizohakikisha tiketi ya mtoano baada ya kushinda mechi zao mbili za mwanzo. Timu nyingine zitalazimika kupigania nafasi kupitia ushindi wa moja kwa moja au nafasi ya timu bora ya tatu.
Katika makundi kadhaa, ushindani bado ni mkali. Morocco, Cameroon na Ivory Coast bado haziko salama, huku timu kama Mali, Zambia, Tunisia na Msumbiji zikiendelea kusaka ushindi wa lazima. Mechi za mwisho zinatarajiwa kujaa presha, hisia na maamuzi ya dakika za mwisho yanayozoeleka kwenye AFCON.
CHANZO: TRT Afrika














