Michezo Afrika Ajenda

AFCON 2025: Simba wa Teranga vs Simba wa Atlas katika fainali ya kihistoria

Ni fainali ya heshima: Senegal kutafuta taji la pili, Morocco kutafuta historia ya miaka 50.

Newstimehub

Newstimehub

16 Januari, 2026

294

Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025) inawakutanisha vigogo wawili wa soka barani: Senegal na Morocco. Ni pambano la kutafuta heshima ya pili kwa Senegal, au historia mpya kwa Morocco baada ya kusubiri kwa nusu karne.

Senegal, mabingwa wa AFCON 2021, wanategemea uzoefu na makali ya Sadio Mané, mshambuliaji mwenye rekodi ya mechi 125 na mabao 53 kwa timu ya taifa. Mané, mwenye umri wa miaka 33, amewahi kung’ara katika ligi za Ulaya na sasa anakipiga Saudi Arabia.

Kwa upande wa Morocco, kumbukumbu ya ubingwa wao wa mwisho ni mwaka 1976, enzi ambazo michuano ilikuwa na timu chache na teknolojia ya kisasa haikuwepo. Leo hii, wanajivunia kizazi kipya kinachoongozwa na Achraf Hakimi wa PSG, beki mwenye kasi na ubunifu, aliyecheza mechi 92 na kufunga mabao 11 kwa timu ya taifa.

Mashabiki wanatarajia Jumapili ya kusisimua, ambapo historia na hadhi ya soka la Afrika itapimwa tena. Kabla ya fainali, Misri na Nigeria watakutana Jumamosi kuwania nafasi ya tatu.

CHANZO: TRT Afrika