Afrika

Afrika Kusini yaanza mjadala wa taifa kutafuta suluhu ya matatizo

Miongoni mwa matatizo ambayo Rais Cyril Ramaphosa ameyataja ni ukosefu wa ajira ambao umepita zaidi ya asilimia 33 na ukosefu wa usawa, ikiwa ni moja ya takwimu mbaya duniani.

Newstimehub

Newstimehub

15 Agosti, 2025

13df8496232166f49dc21fb376c6db5ea696860c21a96fc3c5ad401cabbf2539

Rais Cyril Ramaphosa amewataka raia wa Afrika Kusini kushirikiana kutafuta suluhu kwa matatizo mengi yanayoyakabili nchi, akizindua mchakato wa “majadiliano ya taifa” siku ya Ijumaa ambao wakosoaji waliushtumu.

Mashauriano ya umma kote nchini kwa taifa la Afrika lenye viwanda vingi zaidi ambalo bado linakabiliwa na umaskini mkubwa na ukosefu wa usawa miaka 30 baada ya kumalizika kwa utawala wa ubaguzi wa rangi.

“Sote tunakubaliana kuwa vitu vingi havifanyi kazi katika nchi yetu,” Ramaphosa aliambia mkutano wa watu zaidi ya 1,000 akiweka dira ya mikutano katika maeneo mbali mbali lte nchini katika miezi sita hadi tisa.

“Kwa kuja pamoja, tuzungumze baina yetu, tunaweza kupata suluhu kwa namna ya kuweka mambo mengi sawa hasa yale ambayo hayaendi sawa katika nchi yetu kwa pamoja,” alisema.

Mabadiliko ya masuala ya ardhi

Miongoni mwa matatizo ambayo Rais Cyril Ramaphosa ameyataja ni ukosefu wa ajira ambao umepita zaidi ya asilimia 33 na ukosefu wa usawa, ikiwa ni moja ya takwimu mbaya duniani.

Vipaumbele vilivyoorodheshwa na waandaaji ni pamoja na kiwango cha juu cha uhalifu na mabadiliko katika masuala ya ardhi, huku ardhi kubwa ya kilimo ikiwa bado inamilikiwa na wazungu walio wachache.