Afrika

Ahmed Arajiga kusimama katikati ya dimba kwenye ‘Derby ya Kariakoo’

Mchezo wa ngao ya jamii huashiria kufunguliwa kwa msimu mpya wa mashindano wa 2025-2026, ambao uko chini ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF).

Newstimehub

Newstimehub

16 Septemba, 2025

6548735eef1102042ec091a108766c46932bd01c7f881aa5eb3a3edf43dcbf5d

Refa maarufu nchini Tanzania Ahmed Arajiga, atakuwa mwamuzi wa kati kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii kati ya Yanga SC na Simba Sports Club, utakaofanyika Septemba 16, 2025 jijini Dar es Salaam.

Mwamuzi huyo atakuwa akisaidiwa na Mohammed Mkono, Kassim Mpanga na Ramadhan Kayoko, kwenye mechi hiyo maarufu kama ‘Derby ya Kariakoo’, itakayopigwa kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa.