Afrika

Burkina Faso, Mali, Niger yaanzisha benki ya uwekezaji kufadhili miradi ya miundombinu

Muungano wa Mataifa ya Sahel (AES), yanayojumuisha Mali, Burkina Faso na Niger, yameanzisha benki ya uwekezaji siku ya Jumatano kufadhili miradi mikubwa ya miundombinu na kiuchumi kote katika kanda.

Newstimehub

Newstimehub

18 Desemba, 2025

664ce4d26512b200b476462ec7818153f1ad34a1d0758dfe1f53c06444be8763

Muungano wa Mataifa ya Sahel (AES), yanayojumuisha Mali, Burkina Faso na Niger, yameanzisha benki ya uwekezaji siku ya Jumatano kufadhili miradi mikubwa ya miundombinu na kiuchumi kote katika kanda.

Waziri wa Burkina Faso wa Uchumi, Fedha na Mipango Aboubakar Nacanabo ametangaza kukamilika kwa mchakato wa kuundwa kwa benki hiyo ikianza na mtaji wa dola milioni $895, kufuatia mkutano na mawaziri wa fedha kutoka nchi zote tatu.

AES ilizindua mipango ya kuanzishwa kwa benki ya uwekezaji mwezi Mei 2025 ili kusaidia katika miradi mikubwa na kuimarisha kujitegemea kifedha.