Shirika la Ethiopian Airlines limeeleza kuwa linaweza kuongeza bei za tiketi za ndege iwapo mgogoro unaoendelea Mashariki ya Kati utaendelea kuathiri soko la mafuta.
Afisa Mkuu wa Biashara, Lemma Yadecha Gudeta, amesema kuwa kupanda kwa gharama za mafuta ya ndege tayari kumeanza kuathiri shughuli za shirika hilo, na hali hiyo inaweza kulazimisha mapitio ya bei ili kuhakikisha huduma zinaendelea kwa ufanisi.
CHANZO: TRT Afrika














