Mgombea Urais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania kupitia chama cha wananchi (CUF) Gombo Samandito Gombo amesema serikali yake itaboresha maslahi ya wafanyakazi ili wapunguze makali ya maisha wanayokumbana nayo.
Akizungumza wakati wa kampeni zake katika kata ya Katoro wilayani Bukoba mkoani Kagera, Gombo alisema kuwa chama chake kitahakikisha kinaboresha maslahi ya wafanyakazi ili wapunguze makali ya maisha, hususani yale yaliyosababishwa na uchukuaji holela wa mikopo.
“Sisi CUF tunasema haya maumivu ya maisha waliyo nayo wafanyakazi wetu mpaka ikafika mahali hawatuhudumii vizuri lazima na yenyewe kwa kutumia kodi zetu tuwape wanachostahili ilo waweze kutuhudumia vizuri, “alisema mgombea huyo wa Urais.














