Afrika

Gombo wa CUF aahidi ‘kuwapunguzia’ Watanzania makali ya maisha

Tanzania itafanya Uchaguzi Mkuu wake Oktoba 29, 2025.

Newstimehub

Newstimehub

9 Septemba, 2025

dc955f2daa7da0a15174b26d5565b1456232971ffe3abb25370c5954bac463a3 main

Mgombea Urais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania kupitia chama cha wananchi (CUF) Gombo Samandito Gombo amesema serikali yake itaboresha maslahi ya wafanyakazi ili wapunguze makali ya maisha wanayokumbana nayo.

Akizungumza wakati wa kampeni zake katika kata ya Katoro wilayani Bukoba mkoani Kagera, Gombo alisema kuwa chama chake kitahakikisha kinaboresha maslahi ya wafanyakazi ili wapunguze makali ya maisha, hususani yale yaliyosababishwa na uchukuaji holela wa mikopo.

“Sisi CUF tunasema haya maumivu ya maisha waliyo nayo wafanyakazi wetu mpaka ikafika mahali hawatuhudumii vizuri lazima na yenyewe kwa kutumia kodi zetu tuwape wanachostahili ilo waweze kutuhudumia vizuri, “alisema mgombea huyo wa Urais.