Afrika

Hemetti wa RSF aapishwa kama kiongozi wa serikali sanjari huku raia wakiuawa Kordofan

Jeshi la Sudan linasema watu watano kutoka familia moja, ikiwemo wasichana wawili wadogo, waliuawa kwa shambulio la RSF la ndege zisizo na rubani Kaskazini mwa Jimbo la Kordofan kusini mwa Sudan.

Newstimehub

Newstimehub

30 Agosti, 2025

b4bec93a25da461df849d7a549a963235da23b014d87ecc898c4f70f7d8de636

Mohamed Hamdan Dagalo, kiongozi wa vikosi vya wapiganaji vya Rapid Support Forces, ameapishwa kama kiongozi wa serikali sanjari ya Sudan, serikali imesema katika taarifa, kuelekeza nchi katika hatari ya kugawanyika.

Dagalo, anayejulikana kama Hemetti, hajaonekana sana Sudan tangu kuanza kwa vita vya miezi 28 na jeshi la taifa la nchi hiyo, lakini aliapishwa katika mji wa Sudan wa Nyala, taarifa ilisema. Shirika la habari la Reuters halikuweza kuthibitisha sehemu hasa aliyokuwepo.

Moja ya miji mikubwa ya Sudan, katika eneo la Darfur, Nyala imekuwa kama makao makuu ya RSF, na serikali hiyo imeteua waziri mkuu na baraza la rais, linaloongozwa na Dagalo.

Mji huo ulilengwa na ndege zisizo na rubani siku ya Jumamosi.

Jeshi la Sudan linasema raia watano kutoka kwa familia moja, ikiwemo wasichana wawili wadogo, waliuawa kwa shambulio la RSF la ndege zisizo na rubani Kaskazini mwa Jimbo la Kordofan kusini mwa Sudan.

Mashambulizi hayo ya usiku yalilenga kijiji cha Awlad Al-Sharif katika eneo la Indraba, jeshi lilisema katika taarifa. Wanavijiji wengine sita walijeruhiwa.

Jeshi lilieleza shambulizi hilo kuwa sehemu ya kile walichokiita “muendelezo wa unyama dhidi ya raia na uhalifu wa kivita.” wa RSF

Mashambulizi mabaya