Mohamed Hamdan Dagalo, kiongozi wa vikosi vya wapiganaji vya Rapid Support Forces, ameapishwa kama kiongozi wa serikali sanjari ya Sudan, serikali imesema katika taarifa, kuelekeza nchi katika hatari ya kugawanyika.
Dagalo, anayejulikana kama Hemetti, hajaonekana sana Sudan tangu kuanza kwa vita vya miezi 28 na jeshi la taifa la nchi hiyo, lakini aliapishwa katika mji wa Sudan wa Nyala, taarifa ilisema. Shirika la habari la Reuters halikuweza kuthibitisha sehemu hasa aliyokuwepo.
Moja ya miji mikubwa ya Sudan, katika eneo la Darfur, Nyala imekuwa kama makao makuu ya RSF, na serikali hiyo imeteua waziri mkuu na baraza la rais, linaloongozwa na Dagalo.
Mji huo ulilengwa na ndege zisizo na rubani siku ya Jumamosi.
Jeshi la Sudan linasema raia watano kutoka kwa familia moja, ikiwemo wasichana wawili wadogo, waliuawa kwa shambulio la RSF la ndege zisizo na rubani Kaskazini mwa Jimbo la Kordofan kusini mwa Sudan.
Mashambulizi hayo ya usiku yalilenga kijiji cha Awlad Al-Sharif katika eneo la Indraba, jeshi lilisema katika taarifa. Wanavijiji wengine sita walijeruhiwa.
Jeshi lilieleza shambulizi hilo kuwa sehemu ya kile walichokiita “muendelezo wa unyama dhidi ya raia na uhalifu wa kivita.” wa RSF
Mashambulizi mabaya














