Polisi Tanzania wakiri kumshikilia aliyekuwa Waziri wa Uwekezaji Geoffrey Mwambe
“Hatua zaidi za kisheria zinakamilishwa,”
— Taarifa ya Jeshi la Polisi.
Newstimehub
12 Desemba, 2025
Jeshi la Polisi Tanzania limethibitisha kumkamata na kumshikilia aliyekuwa Waziri wa Uwekezaji na Mbunge wa Masasi, Geoffrey Mwambe, kwa tuhuma za makosa ya jinai yanayochunguzwa. Kwa mujibu wa taarifa ya polisi, Mwambe alikamatwa tarehe 7 Desemba 2025 katika eneo la Tegeta, wilaya ya Kinondoni, na taratibu za kisheria zinaendelea kuchukuliwa.