Kocha mkuu wa Zambia Moses Sichone hawezi kukaa benchi kwani hana sifa zinazohitajika za Shirika la Soka Afrika (CAF), kwa mujibu wa ripoti.
Maafisa wa Chipolopolo (Copper Bullets) wanatarajia kutatua tatizo hilo kwa kumbadilishia cheo cha mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa kuwa kocha msaidizi, kwani anakidhi vigezo vinavyotumika kwa nafasi hiyo.
Zambia wako Kundi A pamoja na Morocco, ambao wanachukuliwa kama wagombea wakuu wa taji, pamoja na Comoros na Mali.
Nigeria imetangaza kwamba kiungo anayekipiga mtanange nchini Uturuki, Wilfred Ndidi, atakuwa nahodha wa timu baada ya William Troost-Ekong, ambaye hivi karibuni alitangaza kustaafu kutoka kwenye mchezo wa kimataifa.
Nigeria watazindua kampeni yao ya Kundi C dhidi ya Tanzania huko Fes, kisha watazikabili Tunisia na Uganda katika mji huo huo.












