Afrika

Mahakama Kenya yapigia msumari sheria ya kustaafu miaka 60

Uamuzi huo ulitolewa katika kesi iliyowasilishwa na raia mmoja, ambaye alidai kuwa kuwataka wafanyakazi kustaafu wakiwa na miaka 60 – au 65 ni ukiukaji wa haki za kikatiba za usawa kwa watu wenye ulemavu.

Newstimehub

Newstimehub

15 Agosti, 2025

1755239609713 tk239 614be943697935f946a5f80e2ffbc5c653117d83d0f3b2acd49114993f6773f9

Mahakama Kuu nchini Kenya imeidhinisha umri wa lazima wa kustaafu kwa wafanyakazi katika sekta ya umma na kibinafsi, ikitupilia mbali ombi lililotaka kutangaza sera hiyo kuwa kinyume na katiba.

Wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi kupitia sheria ya kustaafu ni kati ya umri wa miaka 60, au 65 kwa watu wenye ulemavu, Mahakama Kuu imesisitiza.

Jaji Lawrence Mugambi alitoa uamuzi huo katika kesi iliyowasilishwa na Charles Chege Gitau, ambaye alidai kuwa kuwataka wafanyakazi kustaafu wakiwa na miaka 60 – au 65 kwa watu wenye ulemavu – ni kulikiuka haki za kikatiba za usawa, utu na mazoea ya haki ya kazi.

“Madai kwamba umri wa lazima wa kustaafu … unabagua kwa sababu unawafanya watu katika jamii hiyo kukosa kazi sio sahihi kabisa, ikizingatiwa kuwa sheria na kanuni zinaruhusu mwajiriwa kubakishwa kwa mujibu wa kandarasi,” Jaji Mugambi alisema.