Idadi ya watu waliofariki kutokana na maporomoko ya ardhi kusini mwa Ethiopia imefikia watu 102, kwa mujibu wa maafisa wa eneo hilo.
Tukio hilo lilitokea katika wilaya ya Gacho Baba ndani ya eneo la Gamo baada ya mvua kubwa kunyesha kwa siku kadhaa na kusababisha ardhi kuporomoka katika maeneo ya nyanda za juu.
Ofisi ya mawasiliano ya Gamo imesema hadi sasa miili 52 imepatikana kutoka kwenye vifusi huku juhudi za uokoaji zikiendelea.
Msimamizi wa kanda ya Ethiopia Kusini, Tilahun Kebede, amesema serikali inaendelea kusaidia waathirika na kupeleka misaada katika maeneo yaliyoathiriwa.














