Meta imeanza kuzuia vijana chini ya miaka 16 kutumia Instagram, Facebook na Threads nchini Australia kabla ya sheria mpya kuanza kutumika Desemba 10. Australia inataka majukwaa 10 ya mtandaoni kuwazuia watumiaji wadogo, makampuni yakikabiliwa na faini kubwa endapo watashindwa kutii.
Takribani vijana 350,000 wanaweza kuathirika, huku Meta na YouTube wakipinga sheria hiyo, wakisema inaweza kupunguza usalama. Serikali, hata hivyo, inasisitiza hatua hii inalenga kulinda watoto dhidi ya madhara ya maudhui hatari mtandaoni.











