Mfanyabiashara maarufu wa Tanzania Mohammed Dewji, anayejulikana kama Mo Dewji, ameendelea kuwa tajiri zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati licha ya kushuka kwa nafasi mbili katika orodha ya matajiri barani Afrika.
Jarida la Forbes linaonyesha kuwa Dewji anashika nafasi ya 14 katika orodha ya matajiri wa Afrika, akiwa na utajiri unaokadiriwa kufikia dola bilioni 2.1.
Katika orodha hiyo, mfanyabiashara kutoka Nigeria Aliko Dangote anaendelea kuongoza akiwa na utajiri wa dola bilioni 28.5, huku Johann Rupert na familia yake wakishika nafasi ya pili.
CHANZO: TRT Afrika














