Mfanyabiashara wa Tanzania Rostam Aziz amenunua shirika kubwa zaidi la habari Afrika Mashariki, Nation Media Group (NMG), kutoka kwa familia ya Aga Khan, chombo hicho kilisema siku ya Jumanne.
Mfuko wa Maendeleo ya Kiuchumi wa Aga Khan (AKFED), kupitia kampuni ya NPRT Holdings Africa Limited (NPRT), ulikuwa unamilikia asilimia zaidi ya 54% ya hisa zote za NMG, kufanya AKFED kuwa mwenye hisa nyingi zaidi.
Mfanyabiashara Aziz, 61, kupitia kampuni yake ya Taarifa Limited, amenunua hisa zote za AKFED huko NMG, gazeti la Nation la Kenya limeripoti.
Chanzo: TRT Afrika














