Mwanaharakati mashuhuri wa kupinga utumwa nchini Mauritania, Boubacar Ould Messaoud, amefariki dunia siku ya Alhamisi katika mji mkuu Nouakchott akiwa na umri wa miaka 80.
Kwa mujibu wa mwakilishi wa shirika lake lisilo la kiserikali, taarifa hiyo ilithibitishwa kwa Shirika la Habari la AFP.
Messaoud, aliyekuwa amezaliwa katika familia ya watumwa, alianzisha shirika la SOS Esclaves mwaka 1995 kwa lengo la kupambana na utumwa na kusaidia waliokuwa watumwa kurejea katika jamii.
Shirika hilo lilifanya kazi kwa miaka kadhaa bila kutambuliwa rasmi hadi lilipopata hadhi ya kisheria mwaka 2005.
CHANZO: TRT Afrika














