Mbunge wa Jimbo la Isimani na kiongozi wa muda mrefu serikalini, William Lukuvi, amefariki dunia asubuhi ya Machi 25, 2026 akiwa hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma. Taarifa za kifo chake zimetolewa na Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Katibu Mkuu Kiongozi.
Rais Samia amemuelezea Lukuvi kama kiongozi mwenye uzoefu mkubwa, aliyejitolea kwa dhati kulihudumia taifa. Ameeleza kuwa mchango wake katika maendeleo ya nchi utaendelea kukumbukwa kwa vizazi vijavyo.
CHANZO: TRT Afrika














