Afrika

Rais wa zamani wa DRC Joseph Kabila ahukumiwa kifo

Kabila, ambaye aliiongoza Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kutoka mwaka 2001 hadi 2019, amepinga hukumu hiyo, akisisitiza kuwa mahakama ya nchi hiyo ‘imehadaiwa’ kisiasa.

Newstimehub

Newstimehub

30 Septemba, 2025

68aa4abbc44418ea42d8b0c6a8051194ab8fcdc45e3502f267412eb970f79c7a

Mahakama ya kijeshi nchini DRC imetoa hukumu ya kifo kwa Rais wa zamani wa nchi hiyo, Joseph Kabila baada ya kumkuta na hatia ya uhalifu wa kivita.

Kulingana na Luteni Jenerali Joseph Mutombo, kiongozi huyo wa zamani alipatikana na hatia mbalimbali, ikiwemo uhaini, unyanyasaji wa kingono, mauaji na uhalifu dhidi ya binadamu.

Hata hivyo, Kabila hakuwepo mahakamani wakati wa kutolewa kwa hukumu hiyo, siku ya Jumanne jijini Kinshasa.

Kabila, ambaye aliiongoza Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kutoka mwaka 2001 hadi 2019, amepinga hukumu hiyo, akisisitiza kuwa mahakama ya nchi hiyo ‘imehadaiwa’ kisiasa.

Aliondoka madarakani kufuatia vurugu za kisiasa zilizotokea nchini humo, na amekuwa akiishi Afrika Kusini toka mwishoni mwa mwaka 2023.