Afrika

Rais wa Zanzibar apongeza mchango wa kambi za matibabu

Rais Mwinyi amewahakikishia wananchi kuwa kuwa serikali yake itaendelea kufanya juhudi za kuleta mageuzi katika kuimarisha sekta ya afya.

Newstimehub

Newstimehub

21 Julai, 2025

345c9cf1456df4a21d6766c8131a0185aecac6a925910e6af375354011450b9a

Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa Serikali inatambua mchango mkubwa unaotolewa na kambi za matibabu na uchunguzi wa afya.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo Julai 21, 2025, alipoifungua Kambi ya Matibabu ya Kumbukumbu ya Hayati Ali Hassan Mwinyi, Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja, na kuongezea kusema kuwa kambi hizo zinaisaidia Serikali kupunguza gharama za kusafirisha wagonjwa kwenda kutibiwa nje ya nchi.

46d66533d6247a86d74b43b1c11c89736cbcf9cbb87a278483c310b62a7dbe36 1

Aidha, Rais Mwinyi amewashukuru madaktari bingwa kutoka Kenya na Marekani kwa uamuzi wao wa kuja Zanzibar na kushirikiana na madaktari wazalendo kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi.

Wakati huo huo, Rais Mwinyi amewahakikishia wananchi kuwa kuwa serikali yake itaendelea kufanya juhudi za kuleta mageuzi katika kuimarisha sekta ya afya.

3756bb03a0191725e07637109fc4042631d50282bf0d6c9d8b1c239caf38c17f 1

Amezitaja hatua hizo kuwa ni pamoja na kuimarisha majengo na miundombinu ya sekta ya afya, kuongeza wataalamu wabobezi, pamoja na kuimarisha maslahi yao.