Afrika

Tanzania: Jakaya Kikwete ‘awashangaa’ waliopinga uteuzi wa Samia Suluhu Hassan

Rais huyo mstaafu wa Tanzania, amekosoa hatua ya baadhi ya makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupinga uamuzi wa chama hicho kumpitisha Rais Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea wa chama hicho.

Newstimehub

Newstimehub

29 Agosti, 2025

527e931f11930e07ee7b56c9a427a7847a54c792a86c4ec8791ca72a313896fa

Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete ameoneshwa kushangazwa na baadhi ya watu waliotaka Rais Samia Suluhu Hassan asigombee urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), akihoji kwanini hawakufanya hivyo kwa wakuu wa nchi wa serikali za awamu zilizopita.

Akizungumza Agosti 29, 2025, wakati wa uzinduzi wa kampeni za nchi nzima za chama hicho, zilizofanyika katika viwanja wa Tanganyika Packers jijini Dar es Salaam, Kikwete alidai kuwa wale wanaofanya hivyo, wanafanya kwa makusudi au wanajitoa ufahamu.

“Na mimi nililaumiwa kwa maneno niliyoyasema, na sasa nasema wanaotasema hayo ama wanajisahaulisha au wanajitoa ufahamu. Utaratibu wanaujua na walikuwepo,” alisema kiongozi huyo mstaafu.