Serikali ya Uganda imetangaza sera mpya inayoruhusu raia kutoka mataifa 40 kuingia nchini humo bila viza.
Kwa mujibu wa mamlaka za uhamiaji, wasafiri kutoka nchi zilizoorodheshwa hawatalazimika tena kuomba viza kabla ya kusafiri kwenda Uganda na wataruhusiwa kukaa hadi miezi mitatu kwa ajili ya utalii au shughuli za biashara.
Miongoni mwa nchi za Afrika zilizopewa fursa hiyo ni Kenya, Tanzania, Rwanda, Burundi, Ghana, Zambia, Zimbabwe na Malawi.
Serikali ya Uganda imesema hatua hiyo inalenga kuimarisha ushirikiano wa kikanda, kukuza utalii na kurahisisha biashara kati ya mataifa mbalimbali.
CHANZO: TRT Afrika














