Uturuki

Uturuki inaongoza juhudi za kimataifa katika diplomasia ya kibinadamu na amani – Rais Erdogan

“Tunafanya juhudi kubwa kujenga nchi na eneo lisilo na ugaidi, ghasia,” anasema Recep Tayyip Erdogan.

Newstimehub

Newstimehub

17 Mei, 2025

thumbs b c 8b762b78ae18d152e6b17b17f1fa8fab

Uturuki inaongoza juhudi za kimataifa katika diplomasia ya kibinadamu na amani, rais wa Uturuki amesema kufuatia mazungumzo ya amani kati ya Urusi na Ukraine mjini Istanbul.

Akizungumza katika hafla iliyofanyika Istanbul siku ya Ijumaa, Recep Tayyip Erdogan alisema kuwa Uturuki ndiye “mchukuaji wa kiwango cha diplomasia ya kibinadamu” leo, akiongeza kuwa Uturukii “inaongoza diplomasia ya amani” kote ulimwenguni.

Erdogan pia alisisitiza dhamira ya Uturuki ya kujenga eneo salama na lenye amani akisema: “Tunafanya juhudi kubwa kujenga nchi na eneo lisilo na ugaidi, ghasia na tishio la ugaidi.”

Mazungumzo ya amani ya Istanbul yaliyochukua takriban saa mbili yalihusisha maafisa wa ngazi ya juu wa kisiasa, ulinzi na kijasusi kutoka Urusi, Ukraine na Uturuki.

Waziri wa Ulinzi wa Ukraine Rustem Umerov alithibitisha kuwa kila upande ulikubali kuwaachilia wafungwa 1,000, huku matarajio ya kusitisha mapigano pia yakijadiliwa. Ankara ilisisitiza jukumu lake kama mpatanishi, ikitoa wito wa maendeleo “kwenye njia ya amani.”