Afrika

Zimamoto yapambana kuzima moto katika msitu kaskazni mwa Morocco

Morocco imekuwa na matukio ya moto wa msituni 382 mwaka 2024, na kusababisha uharibifu wa hekta karibu 874

Newstimehub

Newstimehub

13 Agosti, 2025

a5c2dedc1ca2ab7789cbb3c556f4a9e2622078207df9068ccd3e37c17fff052f

Mamlaka nchini Morocco zinaendelea na juhudi za kuuzima moto katika msitu kwa mkoa wa kaskazini wa Chefchaouen.

Kulingana na mwandishi wa shirika la habari la Anadolu, mamlaka zinatumia ndege kuzima moto huo, ulioanza siku ya Jumanne.

Hakuna taarifa zozote za kufariki kwa mtu kutokana na moto huo.

Moto huo ulianza katika msitu wa Dardara karibu na eneo la Chefchaouen huku viwango vya nyuzijoto vikiwa juu sana, afisa mmoja wa Shirika la Taifa la Maji na Misitu la Morocco (ANEF) amesema.

Aliongeza kuwa ndege maalum zilikuwa bado zinafanya kazi kuuzima moto huo.

“Watu katika eneo hilo hawakulala usiku kucha wakiwa wanafanya kazi kuuzima moto huo,” Suleiman Rakib, mkazi mmoja, aliliambia Anadolu.