Mamlaka nchini Morocco zinaendelea na juhudi za kuuzima moto katika msitu kwa mkoa wa kaskazini wa Chefchaouen.
Kulingana na mwandishi wa shirika la habari la Anadolu, mamlaka zinatumia ndege kuzima moto huo, ulioanza siku ya Jumanne.
Hakuna taarifa zozote za kufariki kwa mtu kutokana na moto huo.
Moto huo ulianza katika msitu wa Dardara karibu na eneo la Chefchaouen huku viwango vya nyuzijoto vikiwa juu sana, afisa mmoja wa Shirika la Taifa la Maji na Misitu la Morocco (ANEF) amesema.
Aliongeza kuwa ndege maalum zilikuwa bado zinafanya kazi kuuzima moto huo.
“Watu katika eneo hilo hawakulala usiku kucha wakiwa wanafanya kazi kuuzima moto huo,” Suleiman Rakib, mkazi mmoja, aliliambia Anadolu.














