Afrika

Afrika Kusini yafuzu Kombe la Dunia 2026 baada ya kuifunga Rwanda

Afrika Kusini imekuwa taifa la hivi karibuni kutoka Afrika kufuzu kwa Kombe la Dunia la 2026 baada ya kuichapa Rwanda mabao 3-0 siku ya Jumanne na kuongoza kundi C.

Newstimehub

Newstimehub

14 Oktoba, 2025

e1b6f1d3e3e49943b38a26116c8956492ddb87aa533e7540f57930808ed7e85a

Timu hiyo ya Bafana bafana imefuzu Kombe la Dunia licha ya kuondolewa pointi tatu kwa kumchezesha mchezaji asiyestahili katika mechi za awali.

Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Afrika Kusini kushiriki Kombe la Dunia tangu ilipofuzu moja kwa moja kama mwenyeji mwaka 2010.

Ushindi huo wa Afrika Kusini umeifanya Nigeria kumaliza katika nafasi ya pili kwenye kundi hilo, na sasa italazimika kushiriki hatua ya mchujo ili kufuzu.

Nigeria iliifunga Benin 4-0 nyumbani, baada ya mshambuliaji Victor Osimhen kufunga mabao matatu.