Mashabiki wa soka barani Ulaya wameshutumu FIFA kwa bei “zisizokubalika” za tiketi za Kombe la Dunia 2026, wakizitaja kama “uporaji” na “usaliti wa kihistoria”. Tiketi za fainali katika Uwanja wa MetLife, New York zinauzwa kati ya £3,119 na £6,615, bei ambayo ni mara saba ya gharama za Kombe la Dunia 2022. Hakuna punguzo kwa watoto, na hata mechi za makundi zimepangiwa bei kulingana na umaarufu wa timu. Mashabiki wanataka mauzo kusimamishwa, huku FIFA ikiwa bado haijatoa mwitikio.
CHANZO: BBC NEWS














