Umoja wa Afrika umesitisha uanachama wa Guinea-Bissau kufuatia mapinduzi ya kijeshi

Jeshi la Guinea-Bissau limemteua Jenerali Horta Inta-A kama Rais wa mpito wa nchi hiyo siku ya Alhamisi.
28 Novemba, 2025
RSF nchini Sudan watuhumiwa kuigeuza hospitali ya Kordofan Magharibi kuwa kambi ya kijeshi

Kundi la Madaktari nchini Sudan limesema kwamba wapiganaji wa RSF wameigeuza Hospitali ya Al-Nuhud kuwa kituo cha kijeshi, hatua iliyowalazimu wahudumu wa afya kukimbia na kuwaacha raia bila huduma muhimu.
28 Novemba, 2025
Binti wa Zuma ajiuzulu ubunge Afrika Kusini

Zuma-Sambudla hajatoa ufafanuzi wowote hadharani kuhusu madai ya kuwarubuni watu kuenda kupigana nje ya nchi.
28 Novemba, 2025
Mwanasiasa Adolf Hitler ashinda kwa mara ya 5 mfululizo Namibia

Mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 59 anasema yeye ni tofauti kabisa na dikteta huyo wa Ujerumani, na anapenda atambuliwe kwa jina lake la asili
28 Novemba, 2025

Wabunge wa Afrika Mashariki wapongeza ushindi wa Rais Samia

Rais wa Guinea-Bissau awasili Senegal baada ya jeshi kufanya mapinduzi

Umoja wa Afrika wataka Rais wa Guinea-Bissau aachiwe mara moja

Rais Kagame aishutumu DRC kwa kuchelewesha makubaliano ya amani ya Washington

Kiongozi wa mapinduzi Guinea-Bissau, atangazwa kuwa ‘Rais wa mpito’
27 Novemba, 2025
Mwanamke Mjerumani afungwa jela DRC kwa wizi wa benki
Honorine Porsche kwanza alikiri kuchukuwa pesa lakini baadaye akadai kuwa aliibiwa na maafisa wa usalama walioingia kwenye benki hiyo.

27 Novemba, 2025
Trump aipiga marufuku Afrika Kusini kuhudhuria mkutano wa G20 Miami 2026
Trump ametaja madai “mauaji ya halaiki” dhidi ya wakulima wazungu nchini Afrika Kusini na kukataa kuwapokeza rasmi urais wa G20 kama sababu za kuizuia nchi hiyo kuhudhuria mkutano wa mwakani.

26 Novemba, 2025
Rais wa Nigeria atangaza hali ya dharura kufuatia utekaji uliokithiri
Rais wa Nigeria, Bola Tinubu, ametangaza hali ya dharura ya usalama nchini kote kufuatia msururu wa mauaji na utekaji wa watu.

26 Novemba, 2025
Kiongozi wa jeshi la Sudan atoa wito kwa Trump asaidie kusitisha vita nchini humo
Kamanda wa jeshi la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, ambaye anapigana dhidi ya kikosi hasimu cha wapiganaji wa RSF tangu Aprili 2023, amemwomba Rais wa Marekani, Donald Trump, kusaidia kuleta amani.

26 Novemba, 2025
Jeshi lasitisha mchakato wa uchaguzi nchini Guinea-Bissau, latangaza kuchukua udhibiti
Maafisa wa jeshi wanaojiita “Uongozi wa Juu wa Kijeshi kwa Marejesho ya Utulivu” wamesitisha uchaguzi, vipindi vya vyombo vya habari, huku wakilitaka taifa “liwe na utulivu,” kwa mujibu wa chombo cha habari cha serikali.

26 Novemba, 2025
Hatimaye mlipuko wa volkano ya Hayli Gubbi ya Ethiopia wapungua
Huu ni mlipuko wa kwanza uliorekodiwa wa Hayli Gubbi katika miaka 10,000 iliyopita,” aliambia, na Inawezekana itaendelea kwa muda mfupi na kisha itasimama hadi mzunguko unaofuata.

26 Novemba, 2025
Jeshi la Sudan linasema kuwa limezuia mashambulizi ya RSF kwenye mji muhimu
Jeshi la Sudan lilisema siku ya Jumanne kuwa limezuia mashambulizi ya Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) kwenye mji wa kimkakati wa Kordofan kusini, siku moja baada ya RSF kutangaza kusitisha mapigano kwa muda wa miezi mitatu kwa upande mmoja.

26 Novemba, 2025
Kampuni ya mafuta ya serikali ya Uganda yagundua hifadhi mpya ‘muhimu’
Kampuni ya Kitaifa ya Mafuta ya Uganda (UNOC) inayomilikiwa na serikali imetambua visima tisa vya mafuta katika mtaa wa Kasuruban na “akiba mpya ya mafuta ghafi”, ilisema Jumanne.

25 Novemba, 2025
Wasichana wa shule waliotekwa Nigeria wameachiwa huru
Wasichana 24 waliotekwa katika shule kaskazini-magharibi mwa Nigeria wiki iliyopita wameachiwa huru, msemaji wa gavana wa jimbo la Kebbi alisema siku ya Jumanne.

25 Novemba, 2025
Watu 10 zaidi watekwa nyara Nigeria
Watekaji nyara wamewateka wanawake na watoto 10 katika tukio jipya la utekaji nyara nchini Nigeria, polisi wamesema siku ya Jumanne.



