Sudan yaanza kuijenga upya Khartoum huku vita vikiendelea

Umoja wa Mataifa (UN) inakadiria kuwa ukarabati wa miundombinu muhimu ya mji mkuu utahitaji karibu dola milioni 350, wakati ujenzi mzima wa Khartoum “utachukua miaka.”
21 Agosti, 2025
Uganda yafanya makubaliano na Trump ya kupokea wahamiaji kutoka Marekani

Uganda inakuwa nchi ya Afrika ya mwisho kukubali wahamiaji waliotimuliwa kutoka Marekani baada ya Eswatini, Sudan Kusini na Rwanda.
21 Agosti, 2025
47 wafariki huku maelfu wakiachwa bila makazi kufuatia mafuriko nchini Niger

Maelfu ya watu wamepoteza makazi yao kutokana na mafuriko ambayo yameharibu nyumba na kuua mifugo, kama ilivyosemwa na mamlaka.
21 Agosti, 2025
Watu wasiopungua 22 wanaaminika kufariki katika ajali ya boti Nigeria

Watu wasiopungua 22 wanaaminika kufariki baada ya boti kuzama kaskazini magharibi mwa Nigeria, shirika la huduma ya dharura la nchi hiyo limesema siku ya Jumatano.
20 Agosti, 2025

Mkuu wa UN asema Afrika lazima ifaidike kwanza na madini yake muhimu

Idadi ya vifo yafikia 30 katia shambulio la msikiti Nigeria

Uturuki yaongeza juhudi za kupatikana kwa ‘Libya yenye umoja’

Tanzania: Chama cha CCM kufanya mchakato wa uteuzi wa wagombea ubunge, viti maalumu

Kanya yazindua mradi wa dola milioni 165.5 kurejesha Msitu wa Mau
20 Agosti, 2025
Sudan imeripoti maambukizi 1,575 mapya ya kipindupindu na vifo 22 katika wiki moja
Jumla ya maambukizi yanazidi 101,000, ikijumuisha vifo zaidi ya 2,500 huku janga la afya likizidi kuwa baya katika nchi inayoshuhudia vita vinavyoendelea kati ya jeshi na kikosi cha RSF.

19 Agosti, 2025
Jamhuri ya Afrika ya Kati kufanya uchaguzi mkuu Disemba 28
Wapigaji kura milioni 2.3 wamejisajili kwa ajili ya uchaguzi wa urais, ubunge, serikali za mitaa, na uchaguzi wa manispaa, kulingana na afisa

19 Agosti, 2025
Umoja wa Mataifa washtumu mashambulizi ya ADF yaliyowaua raia 52 Mashariki mwa DRC
Mashambulizi hayo ‘ni ukiukwaji mkubwa wa sheria za binaadamu za kimataifa,’ anasema mkuu wa MONUSCO

19 Agosti, 2025
Watu wasiopungua 25 waokolewa baada ya boti kuzama Nigeria, watu kadhaa bado hawajapatikana
Boti hilo lililokuwa limebeba watu wasiopungua 50 na hakuna miili iliyokuwa imepatikana kufikia Jumanne asubuhi, maafisa wanasema.

19 Agosti, 2025
Somalia inakabiliwa na ongezeko la dondakoo kutokana na uhaba wa chanjo na kupungua misaada
Dondakoo au Diphtheria, ugonjwa wa bakteria unaosababisha kuvimba kwa tezi, matatizo ya kupumua na homa na huathiri zaidi watoto, unaweza kuzuilika kwa chanjo iliyopatikana kwa wingi katikati ya karne ya 20.

19 Agosti, 2025
Zaidi ya magaidi 100 wa al-Shabaab wauawa katika operesheni ya kijeshi ya Somalia
Kitengo cha kijeshi chenye uwezo wa juu, kikiungwa mkono na washirika wa kimataifa, kimefanya operesheni ambayo pia iliharibu maficho ya magaidi.

19 Agosti, 2025
Burhan wa Sudan afanya mabadiliko katika jeshi
Mkuu wa jeshi la Sudan aliteua maafisa wakuu wapya siku ya Jumatatu katika huku akiimarisha udhibiti wa maeneo ya kati na mashariki na kupigana vita vikali magharibi.

19 Agosti, 2025
Waasi waliokuwa na mapanga wameua takriban watu 52 mashariki mwa DRC
Waasi wa ADF waliokuwa na mapanga wamewaua takriban raia 52 katika maeneo ya Beni na Lubero mashariki mwa DRC katika siku za hivi karibuni, maafisa wa Umoja wa Mataifa na mashinani walisema Jumatatu.

18 Agosti, 2025
DRC, waasi wa M23 washindwa kufikia makubaliano ya amani ya Doha
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa M23 wameshindwa kufikia muafaka wa makubaliano ya amani ya Doha katika siku ya mwisho iliyowekwa wao kufanya hivyo.

18 Agosti, 2025
Hamas yakubali mapendekezo ya wapatanishi kusitisha mapigano siku 60 Gaza: Vyombo vya Misri
Kundi la wapiganaji la Palestina Hamas limekubali mapendekezo ya kusitisha mapigano Gaza kwa siku 60 yaliyowasilishwa na wapatanishi wa Misri na Qatar, Vyombo vya habari vya Misri viliripoti Jumatatu.




