25 Aprili, 2025

Mahakama ya Gabon yamthibitisha kiongozi wa kijeshi Nguema mshindi rasmi wa uchaguzi wa urais

Brice Oligui Nguema alipata 94.85% ya kura ikilinganishwa na mpinzani wake mkuu, Alain-Claude By-Nze, aliyepata 3.11%, kulingana na matokeo rasmi ya mwisho.

gabon 20nguema

25 Aprili, 2025

Shirika la Umoja wa Mataifa limefikia watu milioni 4 Sudan lakini linaonya kuhusu njaa kali

Mratibu wa shughuli za dharura anasema Sudan ni nchi pekee ambayo imethibitika kuwa na njaa kali, huku watu milioni 25 wakiwa hawana chakula

sudan

25 Aprili, 2025

Uchunguzi wa huduma za mauzo ya viungo nchini Kenya waanza

Kamati huru itafanya ukaguzi wa kina wa huduma zote za upandikizaji wa figo katika hospitali ya Mediheal iliyopo kaunti ya Eldoret katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, baada ya hospitali hiyo kushutumiwa kwa kuhusika na mauzo ya figo.

2025 03 27t190116z 267822076 mt1usdaynetnp82692649007 frtpip 3 usa today network

25 Aprili, 2025

Rwanda kuanza kutibu wagonjwa bila kuhudhuria vituo vya afya

Hospitali zitatumia teknolojia maarufu kama ‘telemedicine,’ mbinu inayotumia teknolojia ya kidijitali kama vile simu za video, programu za simu na majukwaa ya mtandaoni kutoa huduma za afya kwa mbali.

1745574757675 akch9c gettyimages 1333598807

25 Aprili, 2025

Raia wa Rwanda afunguliwa mashtaka Marekani kwa kuhusika na mauaji ya kimbari

Kama inavyodaiwa katika hati ya mashtaka, Faustin Nsabumukunzi aliyeishi Mareknai tangu 2003, alitumia nafasi yake ya uongozi akiwa Rwanda kusimamia ghasia na mauaji ya Watutsi.

faustin

25 Aprili, 2025

Dunia yaadhimisha siku ya malaria, nchi 9 Afrika bila malaria

Barani Afrika WHO inasema tangu mwaka wa 2000, zaidi ya wagonjwa wa malaria bilioni 1.7 na vifo milioni 12 vimepukwa katika kanda ya Afrika kutokana na juhudi za kimataifa za afya.

africa usaid malaria 78705

25 Aprili, 2025

Marekani kuwa mwenyeji wa makubaliano kati ya Rwanda na DRC

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio atatia saini ‘tamko la kanuni’, siku chache baada ya kutangazwa kusitishwa kwa mapigano kati ya DRC na waasi wa M23 wakati wa mazungumzo ya hivi karibuni yaliyofanywa na Qatar huko Doha.

ap25029494435313

25 Aprili, 2025

Kenya yaamua tena hisabati kuwa somo la lazima

Haya yanajiri baada ya Wizara ya Elimu kutangaza kuwa masomo ya hesabu hayatakuwa ya lazima tena kwa wanafunzi wa sekondari chini ya Mtaala unaozingatia Umahiri (CBC), mabadiliko makubwa kutoka kwa mfumo ulioondolewa wa elimu.

education 1

25 Aprili, 2025

Msumbiji yatangaza kumalizika kwa uasi katika mkoa wenye utajiri wa gesi wa Cabo Delgado

Jeshi linasema limedhibiti kambi za mwisho za mafunzo ambazo bado zilikuwa zinatumiwa na waasi katika mkoa wa kaskazini mwa nchi wa Cabo Delgado.

cabod 20delgado

25 Aprili, 2025

Rais wa Afrika Kusini Ramaphosa kukutana na Trump ‘karibuni’ kusuluhisha matatizo yao

Viongozi hao wawili watajadili kuhusu uhusiano kati ya nchi hizo mbili baada ya serikali ya Trump kusitisha misaada ya fedha kwa Afrika Kusini na kumtimua balozi wao.

trump 20rama
Inapakia...