Mahakama ya UN yakataa kujihusisha na jaji wa Uganda aliyefungwa Uingereza

Mahakama ya Uingereza imesema kama wakili aliyehitimu, jaji wa Mahakama Kuu ya Uganda na jaji wa Mahakama ya Uhalifu ya Umoja wa Mataifa, Lydia Mugambe alielewa sheria na akachagua kuzipuuza.
6 Mei, 2025
Mfululizo wa mashambulizi ya RSF Port Sudan

Vikosi vya Rapid Support Forces, RSF, vinalenga bandari, uwanja wa ndege na kambi ya kijeshi katika mji wa Port Sudan katika mashambulio ya hivi punde ya ndege zisizo na rubani.
6 Mei, 2025
Rais wa Kenya apokea majina ya maafisa walioteuliwa katika Tume Huru ya Uchaguzi

Mwaka 2024 Rais Ruto alishutumiwa na wananchi na wachambuzi wa kisiasa kwa kuchelewa kuunda Tume ya Uchaguzi.
6 Mei, 2025
Wizara ya Sheria Uganda yalaani kuteswa kwa Mwanaharakati aliyefikishwa mahakamani

Mwanaharakati wa upinzani nchini Uganda aliyetoweka ambaye mtoto wa Rais alisema alikuwa anamshikilia alifikishwa mahakamani akiwa anachechemea siku ya Jumatatu.
6 Mei, 2025

Mawaziri watakaoshindwa kuweka wazi mali wanazomiliki kufikia Jumatano watafutwa: Mahama

Mahakama ya kimataifa ya ICJ yakataa kesi ya Sudan dhidi ya UAE kuhusu mauaji ya halaiki

Rwanda inasema inafanya mazungumzo na Marekani ili ipokee wahamiaji

Walanguzi kadhaa wa dawa za kulevya wakamatwa Malawi

Umoja wa Afrika walaani mashambulizi ya Port Sudan
5 Mei, 2025
Uganda yamkamata anayeshukiwa kuwateka nyara watalii baada ya miaka sita
Jeshi la Uganda linasema limemkamata mshukiwa huyo katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrais ya Congo, DRC miaka sita baada ya kuteka nyara watalii.

5 Mei, 2025
Benki Kuu Tanzania yakazia matumizi ya fedha za nchi kwa biashara za ndani
Benki kuu ya Tanzania mapema mwezi huu, imetoa taarifa inayosisitiza matumizi ya fedha za ndani katika manunuzi na biashara zote za ndani huku ikisema kuwa matumizi ya fedha za kigeni ndani ya nchi ni kinyume cha sheria.

5 Mei, 2025
M23 yadhibiti mji wa kimkakati wa wavuvi mashariki mwa DRC licha ya makubaliano ya amani
Waasi wa M23 na washirika wake wachukua udhibiti wa mji wa Lunyasenge magharibi mwa pwani ya Ziwa Edward kaskazini mwa DRC.

5 Mei, 2025
Watatu mbaroni baada ya Rais Ruto kurushiwa kiatu
Rais William Ruto alirushiwa kiatu alipokuwa anawahutubia wakazi wa eneo la Kehancha, kaunti ya Migor siku ya Jumapili.

4 Mei, 2025
Jeshi la Sudan lasema RSF imelenga miundombinu karibu na uwanja wa ndege Port Sudan
Msemaji wa jeshi la Sudan amesema vikosi vya RSF vimelenga kambi ya jeshi la anga na miundombinu mengine karibu na eneo la uwanja wa ndege uliopo Port Sudan

3 Mei, 2025
Idadi ya waliouawa katika shambulizi la Al-Nahud Sudan yafika 300: Tume ya haki
Tume ya kitaifa ya haki za binadamu nchini Sudan imeshtumu ‘ukiukwaji mkubwa uliotekelezwa na vikosi vya RSF dhidi ya raia huko Al-Nahud’

3 Mei, 2025
Gabon kumuapisha kiongozi aliyefanya mapinduzi Oligui kuwa rais
Brice Oligui Nguema alishinda uchaguzi wa mwezi uliopita akipata asilimia 95 ya kura baada ya kuongoza serikali ya mpito kwa miezi 19.

2 Mei, 2025
Mkuu wa Jeshi la Uganda adai kumshikilia mpinzani nyumbani kwake
Mkuu wa jeshi la Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, ambaye pia ni mtoto wa Rais Yoweri Museveni, amefanya msururu wa machapisho kwa X kuhusu mlinzi wa kiongozi mkuu wa upinzani nchini aliyeripotiwa kutekwa

2 Mei, 2025
Kenya yachunguza mauaji ya mbunge Were
Mbunge Charles Were aliuawa jioni ya Aprili 30 jijini Nairobi na watu waliokuwa na silaha ambao inaaminika walikuwa wakimfuatilia, huku taarifa sasa zikisema kuwa alipigwa risasi nne.

2 Mei, 2025
Raia 44 wa Ethiopia waokolewa Afrika Kusini
Kuna visa vya mara kwa mara za raia wa Ethiopia kuingia Afrika Kusini kwa njia zisizo halali hasa kupitia mawakala.




