Serikali ya Benin imethibitisha kukamatwa kwa watu 14 kuhusiana na jaribio la mapinduzi lililofeli Jumapili, tukio ambalo lilihusisha kundi la wanajeshi kutangaza kwenye televisheni ya taifa kwamba wamemwondoa rais Patrice Talon, wamesitisha katiba na kuvunja bunge. Mashirika ya habari yameripoti kuwa wengi wa waliokamatwa ni maafisa wa jeshi. Serikali, ikisaidiwa na sehemu kubwa ya jeshi, iliweza kudhibiti jaribio hilo na kutuliza hofu kuhusu usalama wa rais. AU na ECOWAS zimelaani jaribio hilo, huku Talon akitarajiwa kumaliza muhula wake wa mwisho mwaka 2026.
CHANZO: TRT Afrika














