Jeshi la Anga la Nigeria (NAF) limewaua zaidi ya magaidi 15 wa Boko Haram huko Zuwa, Msitu wa Sambisa, Kaskazini mashariki mwa Nigeria, afisa mmoja alisema Alhamisi.
NAF imewaua magaidi wa Boko Haram zaidi ya 15 siku ya Jumatano kama sehemu ya Kikosi Kazi cha pamoja cha operesheni Hadin Kai cha Kaskazini Mashariki, kulingana na taarifa ya Msemaji wa Jeshi la Anga, Ehimen Ejodame.
Aliongeza kuwa mashambulizi ya anga yanadhihirisha uhakika wa NAF, katika mapambano dhidi ya ugaidi.
“Septemba 3 2025, mpango wa uhakika ulipangwa na kutekelezwa kwa kushambulia eneo jipya la magaidi magharibi mwa Zuwa katika sehemu ya Sambisa.”
‘Maeneo muhimu yameharibiwa’













