Mamlaka ya Chakula na Dawa ya Ghana imeanzisha uchunguzi wa kitaifa kuhusu madai ya uchafuzi wa chips za ndizi zinazouzwa nchini humo.
Uchunguzi huo ulianza baada ya video kusambaa kwenye mitandao ya kijamii ikidai kuwa baadhi ya wazalishaji wanayeyusha plastiki aina ya polyethylene kwenye mafuta ya kukaangia ili kuongeza ukali wa chips na kuongeza muda wake wa kuhifadhi.
Kwa mujibu wa FDA ya Ghana, hatua hiyo inalenga kuthibitisha ukweli wa madai hayo na kulinda afya ya watumiaji.
Mamlaka hiyo imesisitiza kuwa kuyeyusha plastiki kwenye mafuta ya kupikia ni uchafuzi wa moja kwa moja wa chakula na ni hatari kwa matumizi ya binadamu.
CHANZO: TRT Afrika














