Afrika

Idadi ya vifo yafikia 30 katia shambulio la msikiti Nigeria

Serikali imesema kuwa mashirika ya usalama yamepelekwa katika eneo hilo ili kurudisha utulivu.

Newstimehub

Newstimehub

20 Agosti, 2025

7ea9f383360d6a6ea368c3837e2d0907dbce59d639936c0ee2a0dfdb419c108b

Watu wenye silaha wameua takriban watu 30 katika shambulio la msikiti kaskazini magharibi mwa Nigeria, hayo ni kwa mujibu wa mkazi na mbunge wa eneo hilo, na kuongeza idadi ya waliokufa kutoka 13.

“Watu wenye silaha,” makundi ya uhalifu kama wanavyojulikana, wameshambulia msikiti uliopo katika mji wa Unguwar Mantau siku ya Jumanne, katika jimbo la Katsina.

“Waumini tisa waliuliwa hapo kwa hapo na wengine wengi walikufa baadae. Idadi za hivi punde za waliopoteza maisha ni 32,” amesema Nura Musa, mkazi wa eneo hilo siku ya Jumatano.