Kampeni za uchaguzi zimeanza nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati kuelekea uchaguzi mkuu wa Desemba 28, ambapo wapiga kura takriban milioni 2.3 wanatarajiwa kupiga kura katika chaguzi nne kwa wakati mmoja. Rais wa sasa Faustin-Archange Touadera anawania muhula wa tatu, huku upinzani ukilalamikia masharti ya uraia, ucheleweshaji wa uchaguzi na ukosefu wa uwazi katika mchakato wa kura.
CHANZO: TRT Afrika














