Serikali ya North Korea imeonya kuhusu athari zinazoweza kujitokeza kufuatia mazoezi ya pamoja ya kijeshi yanayofanywa na United States na South Korea.
Dada wa kiongozi wa nchi hiyo Kim Jong Un, ambaye ni Kim Yo Jong, alisema mazoezi hayo yanaweza kuongeza mvutano na kusababisha hali ya vurugu katika eneo la Asia Mashariki.
Alisisitiza kuwa North Korea itaendelea kuimarisha uwezo wake wa kujilinda na kukabiliana na vitisho vyovyote kutoka kwa maadui wake.
CHANZO: TRT Afrika














