Mazingira Afrika

Mafuriko ya Afrika Kusini yaacha vifo na kufunga Kruger Park, Mozambique pia yahadharishwa

Mafuriko haya yameacha vifo na kuathiri mamia ya watu, huku Kruger Park ikifungwa.

Newstimehub

Newstimehub

16 Januari, 2026

292

Mafuriko makubwa yaliyosababishwa na mvua za masika kaskazini mashariki mwa Afrika Kusini yamesababisha vifo vya angalau watu 10 na kulazimisha kufungwa kwa Hifadhi maarufu ya Kruger. Katika jimbo la Limpopo, karibu na hifadhi hiyo, watu tisa walipoteza maisha huku takribani 200 wakokolewa na vikosi vya usalama.

Taarifa zinaonyesha kuwa tangu Novemba, jimbo la Mpumalanga limepoteza watu 19 kutokana na mafuriko, na hivi karibuni mwili wa mwanamke aliyesombwa na maji ulipatikana baada ya kujaribu kuvuka mto. Jeshi la taifa lilitoa picha za helikopta zikisaidia wakazi waliokuwa wamekwama juu ya miti.

Mamlaka za hali ya hewa zimetangaza tahadhari ya juu kwa mvua zaidi, na mabwawa makuu yamejaa, hali inayoongeza hatari kwa maeneo ya chini. Rais Cyril Ramaphosa alitembelea Limpopo ili kutathmini uharibifu na hatua za serikali.

Kwa upande wa Mozambique, mamlaka zimeanza kuwahamisha wakazi wa maeneo ya chini kufuatia kuongezeka kwa maji, huku mvua kubwa na upepo mkali ukitarajiwa katika siku zijazo, hata katika mji mkuu Maputo.

Wataalamu wa mazingira wanasema hali hii ya mvua kali na ukame katika maeneo mengine ni ishara ya athari za mabadiliko ya tabianchi zinazoongezeka.

CHANZO: TRT Afrika