Afrika

Mufti Mkuu wa Tanzania ataka utulivu na mazungumzo kuelekea Disemba 9

Mufti Abubakar Zubeir awataka Watanzania kuepuka kauli za chuki

Newstimehub

Newstimehub

8 Desemba, 2025

2672820345565707e70bdaec689140fb5272e36663b1f2f112158a1417724089

Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir, ametoa wito wa utulivu na umoja huku maandamano yaliyopangwa kufanyika Disemba 9 yakiendelea kuzua wasiwasi. Ametaka Watanzania waepuke kauli na matangazo ya chuki, na badala yake waunge mkono mikakati ya mazungumzo na maridhiano. Mufti amesema taasisi za dini zimeanza mazungumzo chini ya usimamizi wa Katibu Mkuu wa BAKWATA kupitia Taasisi ya Tanzania Interfaith Partnership (TIP), yakilenga kuimarisha amani na kulinda maisha na mali za wananchi. Ametoa mwito kwa wananchi kuwa watulivu na kuepuka uchochezi, hasa katika mitandao ya kijamii, akisisitiza kwamba dini zisiruhusiwe kuchochea maandamano yanayoweza kuleta mgogoro.

CHANZO: TRT Afrika