Mshambuliaji wa Nigeria Victor Osimhen ameisaidia Galatasaray kufuzu hatua ya 16 bora ya mashindano ya UEFA baada ya kufunga bao muhimu katika dakika za mwisho za muda wa nyongeza usiku wa Jumatano.
Bao hilo pia limemfanya Osimhen kuwa mfungaji bora wa muda wote kutoka nje ya Ulaya kufunga akiwa na jezi ya Galatasaray katika mashindano ya UEFA. Ingawa Galatasaray ilipoteza mabao 3-2 mjini Turin, matokeo mazuri ya mchezo wa kwanza yaliwapa faida ya kusonga mbele katika mashindano hayo.
CHANZO: TRT Afrika














