Rais wa DRC, Felix Tshisekedi, ameituhumu Rwanda kwa kukiuka makubaliano ya amani yaliyosainiwa tarehe 4 Disemba 2025 nchini Marekani mbele ya Rais Donald Trump. Tshisekedi anadai kwamba siku moja baada ya makubaliano, Rwanda ililishambulia eneo la Kusini mwa Kivu kupitia Bugarama na kusababisha uharibifu katika Kaziba, Katogota na Lubarika.
Rwanda imekana tuhuma hizo, ikizitaja kuwa za “kichekesho”. Machafuko mashariki mwa DRC yameendelea licha ya juhudi za upatanishi kati ya nchi hizo mbili.
CHANZO: TRT Afrika














