Mamlaka za afya nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo zimethibitisha mwisho wa mlipuko wa Ebola katika eneo la Bulape, Kasaï, baada ya siku 42 kupita bila kuripotiwa kesi mpya. Mlipuko huo ulianza Septemba 4 na ulikuwa wa kwanza tangu 2022. Kati ya watu 64 waliothibitishwa kuambukizwa, 45 walifariki na 19 walipona.
WHO imethibitisha kuwa kipindi cha siku 42—sawa na mizunguko miwili ya incubition—kimetimia bila maambukizi mapya, hivyo kuruhusu tamko rasmi la kumalizika kwa mlipuko. Virusi vya Ebola vimeendelea kuwa hatari ya mara kwa mara katika misitu ya tropiki ya Congo, ambako huenea kupitia majimaji ya mwili na kusababisha homa, maumivu ya mwili na kuharisha.














