Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, amesema dunia imeingia kipindi cha machafuko ambapo “sheria ya mwenye nguvu ndiyo inatawala.” Akizungumza Ankara, alionya kuwa baadhi ya mataifa yanakiuka misingi wanayodai kuitetea, na kusema kuwa migogoro inazidi kuhalalishwa na chuki inaenea kimataifa.
Erdogan alisisitiza kuwa Uturuki haiwezi kubaki upande wa kati pale masuala ya amani na usalama yanapohusika. Alisisitiza kuwa migogoro inapaswa kutatuliwa kwa diplomasia na mazungumzo badala ya nguvu, huku nchi yake ikiendeleza mshikamano, ushirikiano, haki na amani duniani. Pia aliongeza kuwa Uturuki haitasaidia vitendo vya uhalifu au mauaji ya halaiki na itashirikiana kuhakikisha watu wanaishi kwa uhuru.
CHANZO: TRT Afrika














