Tanzania: Chama cha CHADEMA chahoji alipo Mwenyekiti wake Tundu Lissu

Lissu anashikiliwa katika gereza la Keko kwa tuhuma za Uhaini zinazomkabili.

Newstimehub

Newstimehub

21 Aprili, 2025

2025 04 11t134647z 710186183 rc2y 4k9uh rtrmadp 3 tanzania politics 1 scaled

Chama cha Demokrasia na Maendeleo nchini Tanzania (CHADEMA) wamelitaka Jeshi la Magereza nchini humo pamoja na vyombo vingine vya dola kueleza alipo Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Tundu Lissu.

Kulingana na taarifa iliyotolewa Aprili 18, 2025 na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA Brenda Rupia, kwa nyakati tofauti, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar Ali Ibrahim Juma, wanachama, mawakili na wanafamilia wamefika katika Gereza la Keko jijini Dar es Salam, ambako anashikiliwa, bila kumuona.

“Hata hivyo, juhudi zao za kumuona Mheshimiwa Lissu hazikufanikiwa baada ya kuelezwa kuwa hayupo katika gereza hilo, cha kusikitisha, hawakupewa maelezo yoyote rasmi juu ya alipopelekwa,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

 Lissu anashikiliwa katika gereza la Keko kwa tuhuma za Uhaini zinazomkabili.