Afrika

Tanzania yatangaza amri ya kutotoka nje Dar es Salaam kufuatia maandamano ya kupinga uchaguzi

Polisi nchini Tanzania wametangaza amri ya kutotoka nje katika mji wa Dar es Salaam kuanzia saa kumi na mbili jioni.

Newstimehub

Newstimehub

29 Oktoba, 2025

7c3b2f920379d1dec366425af643fae7cbcbc0538dfe374fddce1c7d9f7220b0

Amri hiyo imetolewa baada ya kuzuka kwa maandamano ya kupinga shughuli za uchaguzi.

Taarifa ya kutotoka nje imetolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro.

Hapo awali shirika linalofuatilia masuala ya huduma za mitandao duniani, Netblocks limeeleza kuwepo kwa kutatizika kwa huduma za mitandao nchini Tanzania siku ya Uchaguzi Mkuu, ikiwa thibitisho la taarifa za kutokuwepo kwa huduma hizo kama ilivyo kawaida.