Viongozi wa kijeshi wa Guinea-Bissau waliunda serikali Jumamosi, siku chache baada ya kuchukua madaraka kwa njia ya mapinduzi, huku Rais aliyefukuzwa Umaro Sissoco Embalo akiwasili mjini Brazzaville, mji mkuu wa Jamhuri ya Congo.
Jeshi lilichukua udhibiti wa taifa hilo linalozungumza Kireno Jumatano — siku moja kabla ya matokeo ya muda ya uchaguzi wa kitaifa kutarajiwa kutangazwa — na Embalo kwa awali aliondoka kuelekea Senegal jirani.
Jumamosi viongozi wa kijeshi waliteua watu 28, ikiwa ni pamoja na maafisa watano wa jeshi na wanawake wanne, kuongoza taifa hilo la Afrika Magharibi.
Kwengineko mjini Bissau, chama kikuu cha upinzani nchini Guinea-Bissau kilisema makao yake makuu yalivamiwa na watu “waliokuwa na silaha nzito”.
Madhumuni halisi ya mapinduzi nchini Guinea-Bissau bado hayajaeleweka, na uvumi sehemu fulani unaeleza kuwa yalifanywa kwa ridhaa ya Embalo.
Uvumi huo ulizidi kuimarika wakati jeshi lilimteua Jenerali Horta N’Tam, anayechukuliwa kuwa mwenzake wa karibu wa rais aliyefukuzwa, kuongoza mamlaka ya mpito itakayodumu mwaka mmoja.
Jumamosi, N’Tam aliwahimiza serikali mpya “kupigana dhidi ya ufisadi na usafirishaji wa madawa ya kulevya.”
Upinzani nchini Guinea-Bissau umependekeza kwamba Embalo, ambaye amekuwa madarakani tangu 2020, alipanga kuchukua madaraka kwa nguvu ili kumaliza mchakato wa uchaguzi. Embalo bado hajajibu madai haya.
Guinea-Bissau ilifanya uchaguzi tarehe 23 Novemba, na matokeo yalikuwa yatarajiwa kutangazwa tarehe 27 Novemba, lakini siku moja kabla ya tarehe iliyowekwa, mapinduzi yalitokea.
Embalo na mpinzani wake mkuu, Fernando Dias, wote walidai ushindi katika uchaguzi wa hivi karibuni wa urais.














