Afrika

Watu wasiopungua 25 waokolewa baada ya boti kuzama Nigeria, watu kadhaa bado hawajapatikana

Boti hilo lililokuwa limebeba watu wasiopungua 50 na hakuna miili iliyokuwa imepatikana kufikia Jumanne asubuhi, maafisa wanasema.

Newstimehub

Newstimehub

19 Agosti, 2025

981ad9f5970b1b1e46e7e3ba10d6f1fecc8bc241f8936c026d7a5f818963827e

Watu wasiopungua 25 wameokolewa na wengine 25 hawajulikani waliko siku mbili baada ya boti lililokuwa limebeba watu karibu 50 katika Jimbo la kaskazini magharibi la Sokoto, idara ya huduma za dharura imesema siku ya Jumanne.

Mamlaka ya Taifa ya Masuala ya Dharura (NEMA) inasema watu 25 walikuwa bado hawajulikani waliko au pengine wanasemekana kufariki. Hakuna miili yoyote iliyopatikana kufikia Jumanne asubuhi, mamlaka hiyo imesema.

Chombo hicho, ambacho kilikuwa kilikuwa na abiria wanawake, watoto, na pikipiki kuelekea soko la Goronyo, sehemu ya mazao katika eneo hilo, lilipindukia Jumapili, maafisa wanasema.