Uturuki

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Aungana na Mazungumzo ya Awamu ya Pili ya Mpango wa Amani Gaza

Mazungumzo hayo yaliwaleta pamoja maafisa kutoka Marekani, Misri na Qatar kujadili hatua zinazofuata.

Newstimehub

Newstimehub

13 Januari, 2026

258

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Hakan Fidan, ameshiriki katika mkutano wa mtandaoni uliolenga maandalizi ya awamu ya pili ya mpango wa amani wa Gaza.

Kwa mujibu wa wizara ya mambo ya nje ya Uturuki, Fidan alihudhuria kikao hicho siku ya Jumatatu, kama mwendelezo wa mazungumzo yaliyofanyika Miami, Florida, mwishoni mwa Disemba 2025.

Mazungumzo hayo yaliwaleta pamoja maafisa kutoka Marekani, Misri na Qatar, wakijadili hatua zinazofuata katika utekelezaji wa mpango wa amani.

Makubaliano ya kusitisha mapigano Gaza yalianza kutekelezwa tarehe 10 Oktoba chini ya mpango wa vipengele 20 uliowasilishwa na Rais wa Marekani Donald Trump. Hatua hiyo ilisimamisha mashambulizi ya Israel yaliyodumu kwa miaka miwili na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 70,000 na kujeruhi karibu 171,000 tangu Oktoba 2023.

CHANZO: TRT Afrika