FIFA imetangaza mabadiliko mapya ya sheria yatakayotekelezwa katika mashindano ya 2026 FIFA World Cup.
Mabadiliko makubwa zaidi ni kuongezeka kwa idadi ya timu zitakazoshiriki katika mashindano hayo kutoka 32 hadi 48, hatua inayotarajiwa kuongeza ushindani na uwakilishi wa mabara mbalimbali.
Mfumo huo mpya utasababisha pia kuongezeka kwa idadi ya mechi zitakazochezwa katika mashindano hayo.
Kombe la Dunia la 2026 litakuwa la kwanza kufanyika katika nchi tatu kwa pamoja: United States, Canada na Mexico.
Chanzo: Africanews














