Mke wa Rais wa Uturuki, Emine Erdoğan, ametoa wito kwa mataifa kuongeza juhudi za kuhifadhi maji, akisema kuwa maji ni rasilimali muhimu kwa maisha, usalama na uzalishaji wa chakula.
Katika maadhimisho ya World Water Day, amesema dunia inakabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba wa maji, na kusisitiza umuhimu wa matumizi endelevu ya rasilimali hiyo.
CHANZO: TRT Afrika














