Serikali ya Togo kupitia Wizara inayosimamia Nishati na Rasilimali za Madini imetangaza kufanya ukaguzi maalum katika sekta ya machimbo ya vifaa vya ujenzi.
Ukaguzi huo utahusisha tathmini ya kiasi cha malighafi zinazochimbwa, mapato yanayotokana na shughuli hizo, pamoja na ufuataji wa kanuni na sheria za madini.
Kwa ajili ya utekelezaji wa zoezi hilo, serikali imetoa tangazo la kutafuta mshauri (consultant) atakayesimamia na kuendesha ukaguzi huo.
Hatua hii inalenga kuongeza uwazi, kuboresha usimamizi wa rasilimali, na kuhakikisha kuwa sekta hiyo inachangia ipasavyo katika uchumi wa taifa.
Chanzo: Togo First














